Mwenye nyumba yangu anatutoza bei ya umeme kubwa zaidi kuliko TANESCO, nifanye nini?

Wateja wanapaswa kulipa bei ile ile ambayo shirika linatoza,hakuna anaruhusiwa kuuza umeme bila kibali cha mamlaka zinazohusika.Aidha wateja wanashauriwa kuhakikisha maswala yote ya malipo ya umeme au endapo kutakuwa na deni yanaingizwe kwenye mkataba wa pango ili kuondoa sitofahamu ambayo inaweza kujitokeza baadaye.